Tuesday, March 3, 2015

Filamu fupi ya 'KOSA' yaingia production.

Mwongoza na mtayarishaji mahiri wa Filamu hapa nchini Edgar Ngelela anatarajiwa kuachia filamu mpya fupi iliyopewa jina la ‘KOSA’ mwanzoni mwa mwezi wa nne mwaka huu.

Filamu mpya ya 'KOSA'
Ngelela ambaye filamu yake ya awali ya ‘Anguko’ ilipata mafanikio makubwa ya kuoneshwa katika tamasha la kimataifa la 16 la majahazi (ZIFF) huko Zanzibar mwaka 2013, ameiambia Radio Mlimani kwamba filamu hiyo fupi ya ‘KOSA’ inatarajiwa kuwa na urefu wa dakika 25 ikizungumzia maisha ya kila siku.

“Maudhui ya filamu yangu mpya ni maisha ya kila siku lakini zaidi inagusa mapezi, imani na mazoea” alisema Ngelela wakati akizungumza na Radio Mlimani juu ya ujio wa filamu hiyo mpya.

Ngelela ameamua kuiita filamu hiyo ‘KOSA’. Neno hilo la Kiswahili limeubeba ujumbe wa filamu hiyo ipasanyo; kwanza limetumika katika filamu hii likimaanisha kukosa, lakini pia limetumika likimaanisha kukosea, hivyo basi neno hilo limebeba mambo yote mawili katika filamu hiyo fupi, Ngelela alisema.

“Filamu hii ni filamu inayotoa ujumbe kwamba kama mwanadamu ni lazima uwe makini katika kufanya maamuzi, lakini pia kuwaambia watanzania kwamba kila mahusiano ya kimapenzi yana upekee wake” alimalizia mtayarishaji huyo.

Filamu hiyo itakayokamilika mwanzoni mwa mwezi wa nne imelengwa kuoneshwa katika matamasha mbalimbali ya kimataifa na vile vile itapatikana katika DVD hapo baadae.

Miongoni mwa nyota wa filamu hapa nchini waliongára katika filamu hiyo ni pamoja na Bi Madina Hamis maarufu kama dada zawadi pamoja na Emmanuel Myamba anayejulikana zaidi kama Pastor Myamba. Wapo pia waigizaji chipukizi ambapo kwa mujibu wa Ngelela wamefanya kazi kubwa katika filamu hii.

Filamu hiyo imechezewa maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam na pia katika viunga vya mji wa Morogoro.


Na Sylvia Mwehozi, Radio Mlimani.

Wednesday, October 22, 2014

Katiba pendekezwa na Sanaa Tanzania

Leo nizisogeze karibu nanyi wasanii na wasomaji wa blog hii zile ibara tatu ambazo zimejikita kwa namna moja au nyingine kwenye sanaa. Ni vyema kuzipitia na kuzifahamu ili kutoka hapa tujipange vyema kuhakikisha kuwa sheria nzuri zinatungwa ili kuzaa matunda yenye faida kwa wasanii na wananchi kwa ujumla. Ibara hizi ni kama ifuatavyo:

Ibara ya 15: Lengo la taifa kiutamaduni
(1) Lengo la Katiba hii kiutamaduni ni kukuza, kudumisha na kuhifadhi lugha ya Kiswahili, urithi wa asili na utamaduni wa wananchi.
(2) Katika kuhakikisha utekelezaji wa lengo hilo, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili:
(a) kulinda na kuendeleza lugha ya Kiswahili;
(b) kulinda na kuhifadhi urithi wa asili, malikale na sehemu zenye umuhimu wa kihistoria ili kuepuka uharibifu, wizi au utoroshaji nje ya nchi;
(c) kulinda, kuhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii mbalimbali; na
(d) kujenga utamaduni wa kuwepo ushirikiano, maelewano, maridhiano, uvumilivu na kuheshimu mila, desturi na imani ya dini ya kila mtu.

Ibara ya 39: Uhuru wa maoni
Kila mtu:
(a) Ana haki na uhuru wa:
(i) kuwa na maoni na kueleza fikra zake;
(ii) kufanya mawasiliano na kutoingiliwa katika mawasiliano yake; na
(iii) kufanya ugunduzi, ubunifu na utafiti wa sanaa, sayansi na mapokeo ya asili.

Ibara ya 59: Uhuru wa taaluma, ubunifu, ugunduzi, na usanii
(1) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kushiriki kwenye mambo yanayoendeleza na kukuza sanaa, taaluma, ubunifu na ugunduzi.
(2) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kujifunza, kufundisha, kutafiti na kueneza matumizi ya matokeo ya utafiti kulingana na kanuni za kitaaluma na za kiutafiti.
(3) Serikali itakuza na kuendeleza utafiti, ubunifu na ugunduzi katika sanaa, sayansi na teknolojia kwa kutunga sheria ambazo:
(a) zitalinda hakimiliki na hataza na haki za wabunifu, watafiti na wasanii;
(b) zitawezesha taasisi za elimu na za utafiti kutumia ugunduzi wao kwa manufaa ya Taifa;
(c) zitasimamia uhamishaji wa sayansi na teknolojia;
(d) zitawezesha kukuza rasilimali watu kwenye nyanja za kitaaluma, sayansi, teknolojia na ubunifu;
(e) zitalinda na kusimamia ubora wa taaluma, utafiti na matumizi ya ugunduzi na ubunifu; na
(f) zitafafanua mambo mengine yanayohusu hakimiliki na hataza.

Saturday, September 27, 2014

Kituo cha watoto wasioona - Shinyanga


Katika kumuenzi Marehemu Mzee Felix Ngelela Luhende wa Shinyanga anapofikisha miaka minne (4) tangu mauti yake; familia yake ikiongozwa na Mama Hildegard Felix Luhende ilijitoa na kusaidia watoto wasioona, wasiosikia na watoto wenye ulemavu wa ngozi wa kituo cha Blinds kilichopo Buhangija - Shinyanga kwa kuweka plasta na sakafu katika upande mmoja wa bweni moja ambalo lilikuwa halijamaliziwa na bado halitumiki ipasavyo.
Bweni lililowekewa plasta na sakafu
Bweni kabla ya ujenzi wa plasta na sakafu
Bwenini: Ujenzi ukiendelea
Bwenini: Baada ya ujenzi kukamilika
Mpaka siku ya terehe 21/09/2014 kituo kilikuwa kina watoto 276 ambao wanachangia mabweni matatu; la nne likiwa ndio hilo ambalo halijakamilika. Mabweni haya bado hayawatoshi watoto wote kwa pamoja. Hii huwalazimu watoto hao kulala wawili wawili mpaka wanne wanne kwenye kitanda kimoja.
Hivi ni vitanda ambavyo walemavu hulala wawili wawili mpaka wanne
 Ili watoto waweze kuyatumia mabweni haya kwa ufasaha bweni mmoja lina uwezo wa kuwahifadhi watoto 48 lakini kwa hali ya sasa bweni mmoja hubeba watoto 75 mpaka 80 na zaidi, jambo ambalo huwatisha walezi hasa wakifikiria magonjwa ya mlipuko.

Hii iliwafurahisha sana watoto wakitazamia muda si mrefu wengine kuhamia humo na hivyo kupunguza kujaa kwenye mabweni mengine.
Zaidi ya hapo familia ya Mzee Felix Luhende pia iligundua watoto hao walikuwa hawana mahala pa kuanika nguo zao ambapo walilazimika kuanika nguo hizo kwenye madirisha, hivyo familia ikaona ni vema kuwawekea watoto hao kamba kadhaa za kuanikia nguo zao.

Chuma za kufungia kamba za kuanikia nguo zikisubiriwa kukauka
Kituo bado kinahitaji sana misaada mingi kama vile kusaidia kuboresha jiko lao ili kuruhusu hewa zaidi kuingia ndani, kuboresha bwalo lao, kuongeza vitanda na magodoro, chakula na kadhalika. 
Zaidi ya hapo walezi wanahitaji mafunzo zaidi ya malezi na usimamizi ili kuboresha baadhi ya mambo ya msingi katika kuwalea watoto hao.

Friday, March 14, 2014

Meet Maryicker

Keen Insights productions introduces you to the new up coming young artist Maryicker. She is a singer and a dancer from Musoma Tanzania. In introducing Maryicker, Keen Insights in association with Da' voice records brings forth the music video 'Broken heart'. The video is produced by Da' voice records. On the other hand the video is produced by Keen Insights productions.

Maryicker
Maryicker pausing for a photo

Tuesday, February 18, 2014

Anguko film in Hamburg-Germany

The short film 'Anguko' from Tanzania was showcased in Hamburg-Germany. This was in the Valentines day, on February, 14. The film was shown in front of a German and Tanzanian audience at the Golem Cinema hall.
Anguko at the Golem Cinema in Hamburg (A)
Mr. Edgar Ngelela who is the Director of the film said that it was very exiting and quite an experience for him as the film provoked a hot discussion about cultural difference between the two sister cities; Hamburg and Dar es Salaam. He added that although the film told the Hamburgers a lot about the Tanzania culture it gave the Tanzanians who were there a chance to understand the similarities and the difference between the two cultures.
Anguko at the Golem Cinema in Hamburg (B)
The Director was also very thankful to the organizers; Jessica Broscheit and Mark Boombastik Layrer. The film will again be shown at CDEA in Dar es Salaam.

Monday, October 14, 2013

Anguko (The fall) in Arusha at the AAFF

The Short fiction film Anguko has been selected as one of the films that will be showcased in the 2nd Arusha African Film Festival (AAFF). The festival is scheduled to officially open on Friday 29th November, 2013 and close down on Sunday 1st December, 2013.

Edgar Ngelela who is the Producer and Director of the film said that this is an opportunity for the people the people and another chance for those who missed or never had a chance to see the film in the Zanzibar International Film Festival (ZIFF).

Anguko kuoneshwa AAFF Arusha


Filamu fupi ya Anguko imechaguliwa kuoneshwa katika tamasha la kimataifa la filamu za kiafrica ambalo litafanyika huko Arusha. Tamasha hili la Arusha African film (AAFF) linategemewa kufunguliwa rasmi tarehe siku ya Ijumaa 29 Novemba, 2013 na kumalizika siku ya Jumapili tarehe 1 Decemba, 2013.

Edgar Ngelela ambaye ni Producer na Director wa filamu hiyo fupi alikaririwa akisema kuwa hii ni nafasi nyingine ya pekee kabisa kwa watu wa Arusha na wale ambao aidha hawakwenda au hawakupata nafasi kuiona katika tamasha la kimataifa la majahazi la Zanzibar (ZIFF) kuiona.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...