Wednesday, October 22, 2014

Katiba pendekezwa na Sanaa Tanzania

Leo nizisogeze karibu nanyi wasanii na wasomaji wa blog hii zile ibara tatu ambazo zimejikita kwa namna moja au nyingine kwenye sanaa. Ni vyema kuzipitia na kuzifahamu ili kutoka hapa tujipange vyema kuhakikisha kuwa sheria nzuri zinatungwa ili kuzaa matunda yenye faida kwa wasanii na wananchi kwa ujumla. Ibara hizi ni kama ifuatavyo:

Ibara ya 15: Lengo la taifa kiutamaduni
(1) Lengo la Katiba hii kiutamaduni ni kukuza, kudumisha na kuhifadhi lugha ya Kiswahili, urithi wa asili na utamaduni wa wananchi.
(2) Katika kuhakikisha utekelezaji wa lengo hilo, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili:
(a) kulinda na kuendeleza lugha ya Kiswahili;
(b) kulinda na kuhifadhi urithi wa asili, malikale na sehemu zenye umuhimu wa kihistoria ili kuepuka uharibifu, wizi au utoroshaji nje ya nchi;
(c) kulinda, kuhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii mbalimbali; na
(d) kujenga utamaduni wa kuwepo ushirikiano, maelewano, maridhiano, uvumilivu na kuheshimu mila, desturi na imani ya dini ya kila mtu.

Ibara ya 39: Uhuru wa maoni
Kila mtu:
(a) Ana haki na uhuru wa:
(i) kuwa na maoni na kueleza fikra zake;
(ii) kufanya mawasiliano na kutoingiliwa katika mawasiliano yake; na
(iii) kufanya ugunduzi, ubunifu na utafiti wa sanaa, sayansi na mapokeo ya asili.

Ibara ya 59: Uhuru wa taaluma, ubunifu, ugunduzi, na usanii
(1) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kushiriki kwenye mambo yanayoendeleza na kukuza sanaa, taaluma, ubunifu na ugunduzi.
(2) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kujifunza, kufundisha, kutafiti na kueneza matumizi ya matokeo ya utafiti kulingana na kanuni za kitaaluma na za kiutafiti.
(3) Serikali itakuza na kuendeleza utafiti, ubunifu na ugunduzi katika sanaa, sayansi na teknolojia kwa kutunga sheria ambazo:
(a) zitalinda hakimiliki na hataza na haki za wabunifu, watafiti na wasanii;
(b) zitawezesha taasisi za elimu na za utafiti kutumia ugunduzi wao kwa manufaa ya Taifa;
(c) zitasimamia uhamishaji wa sayansi na teknolojia;
(d) zitawezesha kukuza rasilimali watu kwenye nyanja za kitaaluma, sayansi, teknolojia na ubunifu;
(e) zitalinda na kusimamia ubora wa taaluma, utafiti na matumizi ya ugunduzi na ubunifu; na
(f) zitafafanua mambo mengine yanayohusu hakimiliki na hataza.

Saturday, September 27, 2014

Kituo cha watoto wasioona - Shinyanga


Katika kumuenzi Marehemu Mzee Felix Ngelela Luhende wa Shinyanga anapofikisha miaka minne (4) tangu mauti yake; familia yake ikiongozwa na Mama Hildegard Felix Luhende ilijitoa na kusaidia watoto wasioona, wasiosikia na watoto wenye ulemavu wa ngozi wa kituo cha Blinds kilichopo Buhangija - Shinyanga kwa kuweka plasta na sakafu katika upande mmoja wa bweni moja ambalo lilikuwa halijamaliziwa na bado halitumiki ipasavyo.
Bweni lililowekewa plasta na sakafu
Bweni kabla ya ujenzi wa plasta na sakafu
Bwenini: Ujenzi ukiendelea
Bwenini: Baada ya ujenzi kukamilika
Mpaka siku ya terehe 21/09/2014 kituo kilikuwa kina watoto 276 ambao wanachangia mabweni matatu; la nne likiwa ndio hilo ambalo halijakamilika. Mabweni haya bado hayawatoshi watoto wote kwa pamoja. Hii huwalazimu watoto hao kulala wawili wawili mpaka wanne wanne kwenye kitanda kimoja.
Hivi ni vitanda ambavyo walemavu hulala wawili wawili mpaka wanne
 Ili watoto waweze kuyatumia mabweni haya kwa ufasaha bweni mmoja lina uwezo wa kuwahifadhi watoto 48 lakini kwa hali ya sasa bweni mmoja hubeba watoto 75 mpaka 80 na zaidi, jambo ambalo huwatisha walezi hasa wakifikiria magonjwa ya mlipuko.

Hii iliwafurahisha sana watoto wakitazamia muda si mrefu wengine kuhamia humo na hivyo kupunguza kujaa kwenye mabweni mengine.
Zaidi ya hapo familia ya Mzee Felix Luhende pia iligundua watoto hao walikuwa hawana mahala pa kuanika nguo zao ambapo walilazimika kuanika nguo hizo kwenye madirisha, hivyo familia ikaona ni vema kuwawekea watoto hao kamba kadhaa za kuanikia nguo zao.

Chuma za kufungia kamba za kuanikia nguo zikisubiriwa kukauka
Kituo bado kinahitaji sana misaada mingi kama vile kusaidia kuboresha jiko lao ili kuruhusu hewa zaidi kuingia ndani, kuboresha bwalo lao, kuongeza vitanda na magodoro, chakula na kadhalika. 
Zaidi ya hapo walezi wanahitaji mafunzo zaidi ya malezi na usimamizi ili kuboresha baadhi ya mambo ya msingi katika kuwalea watoto hao.

Friday, March 14, 2014

Meet Maryicker

Keen Insights productions introduces you to the new up coming young artist Maryicker. She is a singer and a dancer from Musoma Tanzania. In introducing Maryicker, Keen Insights in association with Da' voice records brings forth the music video 'Broken heart'. The video is produced by Da' voice records. On the other hand the video is produced by Keen Insights productions.

Maryicker
Maryicker pausing for a photo

Tuesday, February 18, 2014

Anguko film in Hamburg-Germany

The short film 'Anguko' from Tanzania was showcased in Hamburg-Germany. This was in the Valentines day, on February, 14. The film was shown in front of a German and Tanzanian audience at the Golem Cinema hall.
Anguko at the Golem Cinema in Hamburg (A)
Mr. Edgar Ngelela who is the Director of the film said that it was very exiting and quite an experience for him as the film provoked a hot discussion about cultural difference between the two sister cities; Hamburg and Dar es Salaam. He added that although the film told the Hamburgers a lot about the Tanzania culture it gave the Tanzanians who were there a chance to understand the similarities and the difference between the two cultures.
Anguko at the Golem Cinema in Hamburg (B)
The Director was also very thankful to the organizers; Jessica Broscheit and Mark Boombastik Layrer. The film will again be shown at CDEA in Dar es Salaam.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...